Recent Post

Tabia za wanyama zenye kuua Taasisi*

*Bata:*
Kujivutavuta, hufanya kazi polepole na kuendekeza uvivu mpaka mambo ya kikundi yanazorota au kufa kabisa.

*Bundi:*
Mtu anayefikiria ana akili kuliko wote kwenye kikundi- hutumia lugha ngumu na haeleweki

*Chura:*
Hurudiarudia kitu kile kile mpaka anawachosha wenzake kundini

*Kenge:*
Hatumii akili sawasawa, ujinga mwingi na hufanya maamuzi ya ovyo yenye kuwakatisha tamaa wenzake

*Kiboko:*
Hulala lala na kupiga miayo. Wakati wenzake wanachacharika yeye ni kukaa tu, hafanyi kazi.

*Kifaru:*
Yeye hushambulia wengine kwenye kikundi bila sababu

*Kinyonga:*
Kigeugeu, akiwa kwa mwanakikundi huyu anasema hili na akiwa kwa mwingine anasema tofauti

*Kobe:*
Hujitoa akiudhiwa, hana uvumilivu kwenye changamoto zinazokabili kikundi.

*Kuku:*
Kuvuruga palipotengenezwa, huenda tofauti na maono ya kikundi kwa kujali na kuzingatia mambo ya muda mfupi tu.

*Mbuni:*
Huficha kichwa na hufikiri hakuna shida kwenye kikundi hata kama zipo shida nyingi

*Nyati:*
Kujihami tu kwa sababu ya woga. Hakosolewi, ukimgusa tu anaazisha vita vya maneno au kupigana

*Nyoka:*
Anajificha huku akiuma bila kusema. Mchonganishi

*Nyumbu:*
Mwoga na hatumii akili kabisa.

*Paka:*
Yeye hutaka ahurumiwe tu na wenzake, hana mchango wowote kwenye kikundi.

*Panya:*
Hachangii chochote yeye hujificha tu na kujitokeza wakati wa neema.

*Popo:*
Hana msimamo. Kwa wanaokubali hoja yupo na kwa wanaopinga hoja yupo! Haeleweki.

*Punda:*
Mgumu kubadilika. Hata umuelimishe vipi, misimamo yake ni ile ile ya zamani.

*Samaki:*
Hachangii hoja, kazi  tu, kukwepa na kutoweka na huonekana hali ikitulia na kuwa shwari.

*Simba:*
Hupigana kama  mawazo yake hakubaliwi na wanakikundi wengine.

*Sungura:*
Hukimbia kama kuna dalili za hatari na kwenda kinyume na makubaliano ya kikundi

*Tausi:*
Yeye huringa kwa mambo mazuri aliyonayo ambayo wanakikundi wenzake hawana.

*Tembo:*
Hufunga njia bila sababu watu wasipite. Huzuia mawazo na maamuzi ya kikundi yasifanikiwe bila sababu.

*Tumbili:*
Mizaha mizaha tu wakati wote hayuko makini hata kwa mambo muhimu ya kikundi.
Share on Google Plus

About JAMPHINA BLOG

0 $type={blogger}:

Post a Comment